Jumanne, Juni 11, 2013

MADADA POA NA CHANGAMOTO WANAZOKUTANA NAZO KATIKA BIASHARA YAO



Kumekuwa na ongezeko kubwa kila kukicha la kina dada wanaojiuza katika maeneo mbalimbali, Na wengi ukizungumza nao na kuwauliza kwanini wameamua kufanya biashara hiyo husema ni kutokana na hali ya maisha kuwa magumu. Hivyo wanaona njia hiyo ni rahisi katika kujiingizia kipato.Nilibahatika kuzungumza na binti mmoja ambaye alionekana kuwa na umri kati ya miaka 15 hadi 17. 

Msichana huyu alikuwa akijihusisha na biashara ya ngono mwenyewe anasema "Niliamua kujiingiza katika biashara ya ngono kutokana na wazazi wangu kufariki na hivyo kukosa msaada kutoka kwa ndugu.Na kwa wakati huo nilikuwa naishi  mkoani Tabora, nikaamua kuja Dar es salaam kutafuta kazi. Nilihangaika sana kutafuta kazi bila ya mafanikio.

 Baadaye nilikutana na dada mmoja  ambaye nilikuwa nikiishi naye na ndiye aliyeniingiza katika biashara hii ya ngono. Nilimuuliza changamoto anazokutana nazo katika biashara hiyo akasema "Kwa siku moja ninaweza nikalala na wanaume zaidi ya watano, kuna wengine hawapendi kutumia kinga, hivyo unakuta anakuongezea pesa kidogo, lakini wengine wanakulazimisha hadi kufanya mapenzi kinyume cha maumbile  na ukikataa anakupiga na hela hakulipi,hizo ni changamoto ninazokutana nazo.

Lakini wanaume wengine wanakulipa tu vizuri" Alisema Binti huyo ambaye alionekana kuchoka sana.Nilimuuliza iwapo kama atapata msaada ili afanye biashara nyingine aachane na  kujiuza akasema "Biashara hii inaniingizia kipato kwa haraka kwa siku naweza kupata kama shilingi elfu hamsini au laki moja  kama biashara ikiwa nzuri, lakini kama nikipata kazi itakayonisaidia kujikimu kimaisha naweza kuacha biashara ya ngono. Kwasasa mimi sina ndugu na hakuna anayenisaidia zaidi ya biashara hii ya ngono.




Hakuna maoni:

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

share bottom