Ijumaa, Aprili 11, 2014

SOMA MANENO HAYA MAZURI KATIKA CHANGAMOTO ZA MAISHA........


Usikate tamaa  fikiria, ulipotokea na unapokwenda,embu tizama wewe unauwezo wa kula  chakula mara tatu kwa siku, kuna ambao hawajui hata huo mlo mmoja kwa siku watapata wapi. Usiishi maisha ya kukufuru na kulalamika, juhudi zako ndiyo mafanikio yako bila kukata tamaa.
 *****************************************************
Usiogope, kufanya jambo fulani kwa hofu ya kuwa utashindwa au kufikiria je watu watasema nini, fanya jambo unalotaka kufanya huku ukiwa na matumaini ya kushinda ikitokea umeshindwa basi utakuwa umejifunza nini cha kufanya ili usirudie kosa kwa mara nyingine,, kumbuka asiyekubali kushindwa si mshindani.
******************************************************
Hakuna mafanikio bila changamoto, kidogo ulichonacho ndiyo mwanzo wa kuwa na kikubwa unachokitamani, kitumie hicho kidogo upate kikubwa, kumbuka ata mbuyu ulianza kama mchicha. 

Hakuna maoni:

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

share bottom