Jumatano, Mei 21, 2014

MUHIMU SANA KUFAHAMU HILI KWA AFYA "Je Saratani ya Tezi-Kibofu ni 'maradhi ya Zinaa?'

Hii ni kwa mujibu wa wanasanyansi nchini Marekani. Wanasema kwamba Saratani hiyo husababishwa na maradhi fulani ambayo huenezwa wakati wa kitendo cha ngono.
Lakini wataalamu wanasema kuwa ushahidi bado haupo kama kweli Saratani hiyo ni moja ya magonjwa ya zinaa na inasababishwa na magonjwa ya zinaa.
Ingawa baadhi ya Saratani husababishwa na maradhi fulani fulani, kitengo cha utafiti wa Saratani nchini Uingereza kinasema kuwa ni mapema mno kuongeza Saratani ya tezi kibofu kwa Saratani hizo.
Wanasayansi waliofanya utafiti huo walichunguza celi za tezi kifobu cha binadamu katika maabara.
Waligundua kuwa maradhi ya zinaa yaitwayo, 'Trichomoniasis' yalichochea ongezeko la Saratani hiyo.
Hata hivyo mfumo wa maisha pia unachangia ongezezeko la visa vya magonjwa ya Saratani.
Ugonjwa wa 'Trichomoniasis' unaaminika kuwaathiri watu milioni 275 duniani na moja ya maradhi maarufu ya Zinaa ambayo hayasababishwi na Virusi


'Dalili za Trichomoniasis'
Kawaida, mtu hatapata dalili za ugonjwa huo na inawezekana asijue kama anaugua ugonjwa huo.
Wanaume huhisi kujikuna sana ndani ya uume wao , kupata hisia za kuchomeka wakati wanapokwenda haja ndogo au kuvuja majimaji meupe kutoka kwa uume wao.
Wanawake pia wana hisia tu sawa na hizo katika sehemu zao za isiri pamoja na kuwa na harufu mbaya
Utafiti huu wa hivi karibuni sio wa kwanza kuhusisha ugonjwa wa 'Trichomoniasis' na Saratani ya Tezi kibofu.
Utafiti uliofanywa mwaka 2009 ulipata kuwa robo ya wanaume walio na Saratani hio walikuwa na dalili za ugonjwa wa Trichomoniasis na wanaume hawa pia walikuwa na uvimbe ambao ulikuwa umekomaa mno.
'Hoja ya Uchunguzi zaidi'
Uchunguzi huo pia unaonyesha njia ambazo ugonjwa huo wa zinaa unawaweka wanaume katika hatari ya kupata Saratani ya tezi kibofu.
Profesa Patricia Johnson na watafiti wenzake, waligundua kuwa viini vinavyosababisha ugonjwa wa 'Trichomonas vaginalis' - huvuja proteni ambayo husababisha Saratani ya Tezi Kibofu kuzuka.
Mtaalamu wa afya, Nicola Smith,anasema uchunguzi huu unaonyesha tu njia ambazo ugonjwa wa zinaa wa Trichomonas vaginalis unazidisha uwezo wa mtu kuugua Saratani ya Tezi Kibofu na kuchochea seli kukuwa kwa kasi.
"Lakini uchunguzi huu ulifanywa tu katika maabara na matokeo ya awali kwa wagonjwa yalikosa kuonyesha uhusiano kati ya ugonjwa huo na Saratani ya Tezi Kibofu,'' alisema Bi Nicola
Kwa kauli hii wanasema kuwa uchunguzi zaidi unahitajika ili kuabini hasa kinacho sababisha Saratani ya Tezi kibofu kwani ugonjwa wa Trichomoniasis husababisha tu mazinigira kwa ugonjwa huo kukomaa ila sio chanzo cha ugonjwa wenyewe.NA BBC SWAHILI

Hakuna maoni:

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

share bottom