Jumatano, Juni 04, 2014

INSTAGRAM YAFUTA NA KUDELETE KABISA PICHA ZA UTUPU.

Mmoja wa waasisi wa mtandao wa kijamii wa Instagram, amesema kuwa sheria zake kuhusu picha za utupu hazimbagui mtu yeyote baada ya mtandao huo kuamua kuondoa picha za utupu. Afisa mtendaji wa mtandao huo, Kevin Systrom alisema sheria hizo zinalenga kuhakikisha kuwa vijan na watu wazima wanaotumia mtandao huo wanakuwa salama, Masharti ya mtandao huo yanasema mtu harusiwi kuweka picha za watu walio nusu uchi na picha zenye mada ya ngono.
Afisa mtendaji mkuu wa mtandao wa kijamii wa Instagram, Kevin Systrom, ambaye anadaiwa kufuta picha za uchi kwenye mtandao wa Instagram
 "Tunapaswa kuwa na sheria na kuhakikisha kuwa kila mtu anazifuata sheria hizo . Bila shaka tunapata changamoto nyingi lakini tutaendelea kusisitiza umuhimu wa sheria kutafutwa. Alisema Systrom.

Hakuna maoni:

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

share bottom