Alhamisi, Juni 12, 2014

POLENI SANA WAFANYABIASHARA WOTE WA KARUME MLIOPATWA NA MAJANGA HAYA

 Moto mkubwa umetetekeza kabisa soko kubwa la mitumba la karume Dar es Salaam usiku wa Jumatano, na kusababisha hasara kubwa kwa wafanyabiashara wote wa soko hilo.
 Wazima moto walifanikiwa kuudhibiti moto uloweza kufikia karibu na kiwanda cha kutengeneza bia cha Breweries, lakini haujasababisha hasara yeyote katika nyumba za jirani wa soko hilo kufuatana na mwandishi habari wa Raia Mwema Mbaraka Islam alipozungumza na Sauti ya Amerika.

Hakuna kibanda cha biashara kilichosalimika na hakuna mtu aliyefanikiwa kuokowa mali yake. Mfanya biashara Wilson magembe anasema amepoteza kila kitu na ilikuwa vigumu kuweza kuchukua bidhaa zao kwa sababu moto uliwaka kwa haraka sana.
wolpergambe Poleni wafanya biashara wote wakarume mlopatwa na majanga haya masikn mtaji wa masikin ni nguvu zake... sasa kma mtu alikopa au aliuza ktu apate mtaji ndo hvyo tena dah maisha haya bwana ...embu tuwaombee hawa wenzetu jamani ..ninaimani wengne hyo hyo biashara ndo mtoto anapata kwenda shule lkn ndo basi tena mtu anaanza upya...serkali hvi vyombo vya zima moto viongezwe basi naviwe vinakaa sehem mbalimbali kama sokon,nk...Mungu tutangulie na wabark viongozi wetu walione hili...Amen

Hakuna maoni:

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

share bottom