Jumatatu, Juni 08, 2015

UJUMBE WA LEO NA DINA MARIOS "Tunaishi katika dunia ambayo binadamu wamekosa utu na imani"


'Katika haya maisha hamna kitu kibaya kama kumuonea na kumnyanyasa mtu ambaye hana hatia.Kwa kutumia cheo,madaraka,nguvu na nafasi uliyonayo ukiamini huyo mtu hana uwezo wa kukufanya lolote

Tunaishi katika dunia ambayo binadamu wamekosa utu na imani.Binadamu wamekuwa wanyama na makatili kuliko wanyama wenyewe.Unaweza ukakutana na simba na chui porini mkakaa mkatia story lakini sio binadamu.

Unafanyiwa unyama eti kisa wanataka revenge kwa mtu wako wa karibu.Ambae revenge hiyo wala haimuathiri lolote zaidi ni kukutesa wewe kisaikolojia siku hadi siku.
Mbaya zaidi sikustahili miaka yote nimejituma,nimejitoa,sijawahi kumvunjia heshima alokuwa juu yangu kwa ngazi zoote.


Ndugu zangu nimeishi kwa muda mrefu katika huzuni,msongo wa mawazo.Na hapa niliponimedevelop na vidonda vya tumbo.Nimekuwa na kitu kifuani kimenikaaa kila siku nahisi nisiposema nitakufa.Ningekuwa nimetendewa haki isingeniuma wala kunisumbua ni kwa sababu nimeonewa sanaa tena katika kipindi kibaya sana.

All this time nimekuwa mnyenyekevu na najichekesha nakujitabasamisha machoni pa watesi wangu.Na wao wakiendelea kunikanyagia chini bila huruma huku wakinichekea.

Leo nimeamka nina huzuni sana sana na ninahuzunika hasa ninapokutana na msg za kuniuliza niko wapi?mbona sisikiki??
Mimi bado ni muajiriwa na ninalipwa mshahara ila nimewekwa benchi tu.

Kuna kitu naomba nikiweke clear kumekuwa na maneno mengiiiiii yanazunguka kuwa nina ugomvi na Zamaradi.Mimi sina ugomvi na Zamaradi sijui ndio amechangia mimi kutolewa kwenye leo tena.Thats not true wala nguvu hiyo hana.Sijajua why watu husema hivyo ila sina ugomvi nae.Hata yeye anajua hatuna ugomvi wowote.Nilipotoka pale niliamua kubadili mfumo wangu wa maisha hivyo hatuna ukaribu kama zamani.Ila haimaainishi tuna ugomvi.

Na malizia kwa kusema sipo radio wala sipo tv kwa sasa.Maswali mnaniuliza kila siku na nina wajibu kila mara na leo nimewajibu tena.
ila nitakuwa kwa radio na tv hapo baadae acha niuze mafuta ya nazi.Maelezo ya mwanzo yamejitosheleza sanaa na sitaenda mbalii sanaa labda nikiandike kitabu ndio yatatimia.

Nimeandika haya kwa ufupi mjue hata sisi pamoja na majina tuliyonayo changamoto zipo na tunakabiliana nazo.Na ipo siku tutashinda maana mtetezi wetu yu hai ' Dina Marious

Maoni 1 :

emu-three alisema ...

Mhh pole sana mpendwa kumbe tupo wengi, lakini usijali, yote na maisha na mungu ndiye mpaji, tupoo pamoja

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

share bottom