Jumatatu, Januari 18, 2016

"Jisamehe makosa yako kwa kusahau yaliyopita uishi kwa amani"

Katika maisha hakuna binadamu aliyekamilika na kutenda makosa ni jambo ambalo linatokea katika maisha yetu ya kila siku, wakati mwingine, huwa tunahuzunika na kujuta makosa tuliyotenda na kwa wakati huo inakuwa tayari umechelewa kurekebisha ulipokosea bali yanabaki majuto kama "yalaiti nisingefanya hivi ama vile".

 Hivyo ili uweze kuendelea kuishi maisha ya amani ni muhimu kuomba msamaha kwa Mungu pamoja na wewe mwenyewe kujisamehe makosa yako. Pia kuwasamehe waliokokosea ikiwa na wewe kuwaomba msamaha waliokukosea waswahili husema "yaliyopita si ndwele tugange yajayo".

Hakuna maoni:

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

share bottom