Wednesday, June 19, 2013
SIMULIZI YA KOSA LANGU NI NINI.....SURA YA ....8.....
ILIPOISHIA
Siku moja alikuja na mwanamke hadi nyumbani. Ilikuwa ni usiku wa saa nne ambapo Joyce alikuwa bado hajalala akimsubiri Maliki arudi, mara Maliki akaingia na huyo mwanamke huku wakiwa wamekumbatiana Joyce hakuamini alichokuwa anakiona kwa mshangao alisema "Heee! Maliki! huyu ni nani?" Masikini Joyce misukosuko inazidi kumuandama. JE NINI KITAENDELEA USIKOSE SURA YA ....8......
INAPOENDELEA
Wakati Joyce akiwa anashangaa kumuona Maliki akiwa na mwanamke tena huku
wakiwa wamekumbatiana na kupeana mabusu motomoto. Bila ya kujali chochote, Maliki
alimgeukia Joyce na kusema "Hivi wewe una mamlaka gani ya kuniuliza huyu
ni nani?" Joyce alimjibu kwa sauti ya upole "Kweli Maliki unanijibu kama
hunijui? Nimekukosea nini mimi, unanifanyia yote haya. Umeona haitoshi kuwa
na wanawake nje, umeamua kuwaleta kabisa na hapa ndani".
Kwa dharau yule mwanamke aliyekuwa na Maliki alicheka na kumtizama Maliki huku akiwa anamshika kwenye paji la uso wake. "Mpenzi nimechoka sana jamani, huyu naye ni nani? Mbona anaongea sana" Alisema yule mwanamke huku akionekana kujishebedua kwa maringo. Joyce kusikia hivyo alishikwa na hasira na kumsogelea yule mwanamke kwa nia ya kumpiga "Wewe unauliza mimi ni nani? mwendawazimu mkubwa usiye kuwa na haya kuchukua mabwana za watu" alisema Joyce huku akiwa amemkamata yule mwanamke ambaye alionekana ana umbo kubwa kuliko la Joyce. Wakati akiwa anafanya hivyo Maliki alimvuta na kumsukuma maskini Joyce alianguka chini huku akiwa analia kwa uchungu .
Kwa dharau yule mwanamke aliyekuwa na Maliki alicheka na kumtizama Maliki huku akiwa anamshika kwenye paji la uso wake. "Mpenzi nimechoka sana jamani, huyu naye ni nani? Mbona anaongea sana" Alisema yule mwanamke huku akionekana kujishebedua kwa maringo. Joyce kusikia hivyo alishikwa na hasira na kumsogelea yule mwanamke kwa nia ya kumpiga "Wewe unauliza mimi ni nani? mwendawazimu mkubwa usiye kuwa na haya kuchukua mabwana za watu" alisema Joyce huku akiwa amemkamata yule mwanamke ambaye alionekana ana umbo kubwa kuliko la Joyce. Wakati akiwa anafanya hivyo Maliki alimvuta na kumsukuma maskini Joyce alianguka chini huku akiwa analia kwa uchungu .
Labels:
KOSA LANGU
Tuesday, June 18, 2013
Monday, June 17, 2013
SIMULIZI...BADO MIMI...SURA YA .........22.......
ILIPOISHIA
Haukupita muda
nilipata mpangaji mwingine ambaye hakuishi muda mrefu alifariki baada ya
miezi
miwili tokea ahamie ile nyumba. Kutokana na
hali hiyo baadhi ya watu walianza kuzungumza maneno mengi kuwa ile
nyumba ina mambo ya kishirikina kwani
kila mtu atakayeishi pale basi lazima katika familia yake kuna mtu
atakufa. JE NINI KITAENDELEA USIKOSE ......SURA YA ...22......
INAPOENDELEA
Hali ile ilinifanya nikose amani, kwani
wapangaji kama watano walihama kutokana na matatizo wanayokutana nayo, kwa nyakati tofauti. Siku moja
nilienda kanisani kwenda kumueleza
Mchungaji Mkombozi hali halisi ya mauzauza ya ile nyumba.Kutokana na matatizo yaliyokuwa yanatokea, nilikuwa na
wasiwasi huenda Mama Bilionea kuna vitu alivificha kule ndani hatukuviona.
Nilipofika kwa Mchungaji nilimkuta akizungumza na kaka mmoja ambaye alionekana
kuwa mgeni pale kanisani alinisalimia “Habari yako dada, mimi naitwa Charito
sijui mwenzangu unaitwa nani,” Nilimtizama yule kaka alionekana mcheshi "Salama tu kaka mimi naitwa Kandida" Huku akitabasamu akanijibu "Nimefurahi sana kukufahamu Kandida" Hahahahahahah "Kilikuwa ni kicheko cha Mchungaji "Karibu Kandida, huyu kijana ni muumini mpya ambaye tutakuwa naye kanisani. Charito naona ulipomuona Kandida umeonyesha tabasamu pana sana" Alisema Mchungaji huku akimtizama Charito.
Nilisogea karibu na kuketi Charito alinyanyuka na kutoka nje na kutuacha mimi na mchungaji, nilimueleza kila kitu mchungaji akasema "Hapana, haiwezekani shetani kushindana na nguvu za Mungu, na hao wanaosema bado kuna mambo ya kishirikina ni akina nani? Mimi namtumainia Mungu wangu pekee na naimani atapambana na nguvu yoyote ya giza" Aliongea mchungaji huku akiwa ananitizama. Tulianza kukemea palepale katika ofisi ya mchungaji na baadaye tukaenda pamoja katika nyumba ya Mama Bilionea safari hii tulikuwa pamoja na Charito.
Labels:
BADO MIMI
Sunday, June 16, 2013
DADA POA..DADA POA....DADA POA COMING SOON
| Baada ya simulizi ya HAKUNA SIRI.... AMBAYO ITAISHA WIKI IJAYO......SIMULIZI YA DADA POA SI YA KUKOSA KUISIKILIZA HAPAHAPA KIJIWENI KWETU. |
Labels:
DADA POA
SIMULIZI ....KOSA LANGU NI NINI.....SURA YA ......7.......
ILIPOISHIA
kesho
ujiandae nitakupeleka Hospitali asubuhi kwenda kuitoa hiyo
mimba" aliongea Maliki huku akiwa anaondoka na kumuacha Joyce akiwa
analia
pale sebuleni huku moyoni akiwaza "Kwanini mimi naishi maisha ya tabu
hivi, nilijua Maliki ananipenda jamani
nimemkosea nini Mungu laiti wazazi wangu wangekuwepo, sijui nitafanya
nini na Maliki ndiyo anataka nitoe hii mimba si nitakufa mimi jamani"
Alisema Joyce kwa uchungu. JE NINI KITAENDELEA... USIKOSE ...SURA YA
...7.....
INAPOENDELEA
Wakati huo ilikuwa mida ya saa nane za mchana. James mdogo wake na Joyce
alikwa ametoka shule na kumkuta Joyce akiwa analia. James alishtuka kabla hata
ya salamu alimuuliza "Dada unamatatizo gani? Mbona unalia kuna nini
kimetokea" Dada yake alivuta kanga aliyokuwa ameivaa na kujifuta machozi
huku akimwangalia mdogo wake kwa huzuni
"Hakuna kitu mdogo wangu nimewakumbuka sana wazazi wetu" Alisema Joyce ambaye siku zote alikuwa hapendi mdogo wake ajue kama anateseka.
James alimshika mkono dada yake na kumwambia "Usilie dada
hata mimi nawakumbuka sana lakini hatuna jinsi inabidi tumshukuru Mungu shemeji
Maliki anatusaidia sana, bila yeye tungekuwa tunaishi mitaani."Akiwa
anazungumza James alimkumbatia dada yake na baadaye aliingia chumbani
kubadilisha nguo na kuendelea na mambo mengine.Siku hiyo ilikuwa ni siku mbaya
sana kwa Joyce ambaye alikuwa hana amani muda wote alikuwa mwingi wa mawazo
ilipofika usiku Maliki alirudi na kumkuta Joyce akiwa tayari amelala. Alimsogelea kwa umakini huku akiwa anamuangalia moyoni mwake aliwaza
"Mmmmh leo nimegombana sana na huyu mtoto ngoja nimuamshe
nimbembeleze".
Alimsogelea tena kwa ukaribu zaidi na kumgusa paji la uso huku akimuamsha taratibu, Joyce aliamka na kumwangalia na macho yaliyokuwa yamelegea kutokana na usingizi. Maliki akamuambia embu amka tuzungumze kidogo, Joyce aliamka na kuketi kitandani.
Alimsogelea tena kwa ukaribu zaidi na kumgusa paji la uso huku akimuamsha taratibu, Joyce aliamka na kumwangalia na macho yaliyokuwa yamelegea kutokana na usingizi. Maliki akamuambia embu amka tuzungumze kidogo, Joyce aliamka na kuketi kitandani.
Labels:
KOSA LANGU
LEO NI SIKU YA MTOTO WA AFRICA
![]() |
| WATOTO KATIKA GARI WALILOTENGENEZA WENYEWE |
![]() |
| WATOTO WAKIIMBA KWA FURAHA |
![]() |
| WATOTO HAWA WANAHITAJI MSAADA ILI WAPATE HAKI YA MSINGI YA KUPATA ELIMU NA KUEPUKANA NA AJIRA ZA UTOTONI |
Subscribe to:
Posts (Atom)











