Wednesday, June 19, 2013

VOTE NANDO VOTE NANDO ...AENDELEE KUBAKI KATIKA JUMBA LA BIG BROTHER


SIMULIZI YA KOSA LANGU NI NINI.....SURA YA ....8.....



 ILIPOISHIA
Siku moja alikuja na mwanamke  hadi nyumbani. Ilikuwa ni usiku wa saa nne ambapo Joyce alikuwa bado hajalala akimsubiri Maliki arudi, mara Maliki akaingia na huyo mwanamke huku wakiwa wamekumbatiana Joyce hakuamini alichokuwa anakiona kwa mshangao alisema "Heee! Maliki! huyu ni nani?" Masikini Joyce misukosuko inazidi kumuandama. JE NINI KITAENDELEA USIKOSE SURA YA ....8......

INAPOENDELEA 

Wakati Joyce akiwa anashangaa kumuona Maliki akiwa na mwanamke tena huku wakiwa wamekumbatiana na kupeana mabusu motomoto. Bila ya kujali  chochote, Maliki alimgeukia Joyce na kusema "Hivi wewe una mamlaka gani ya kuniuliza huyu ni nani?" Joyce alimjibu kwa sauti ya upole "Kweli Maliki unanijibu kama hunijui? Nimekukosea nini mimi, unanifanyia yote haya. Umeona haitoshi kuwa na wanawake nje, umeamua kuwaleta kabisa na hapa ndani".

 Kwa dharau yule mwanamke aliyekuwa na Maliki alicheka na kumtizama Maliki huku akiwa anamshika kwenye paji la uso wake. "Mpenzi nimechoka sana jamani, huyu naye ni  nani? Mbona anaongea sana" Alisema yule mwanamke huku akionekana kujishebedua kwa maringo. Joyce kusikia hivyo alishikwa na hasira na kumsogelea yule mwanamke kwa nia ya kumpiga "Wewe unauliza mimi ni nani? mwendawazimu mkubwa usiye kuwa na haya kuchukua mabwana za watu" alisema Joyce huku akiwa amemkamata yule mwanamke ambaye alionekana ana umbo kubwa kuliko la Joyce. Wakati akiwa anafanya hivyo Maliki alimvuta na kumsukuma maskini Joyce alianguka chini huku akiwa analia kwa uchungu .


HAYA NAYO NI MANENO MAZURI KATIKA CHANGAMOTO ZA MAISHA




Tuesday, June 18, 2013

Monday, June 17, 2013

SIMULIZI...BADO MIMI...SURA YA .........22.......





 ILIPOISHIA
Haukupita muda nilipata mpangaji mwingine ambaye hakuishi muda mrefu alifariki baada ya miezi miwili tokea ahamie ile nyumba. Kutokana na  hali hiyo baadhi ya watu walianza kuzungumza maneno mengi kuwa  ile nyumba ina mambo ya kishirikina kwani kila mtu atakayeishi pale basi lazima katika familia yake kuna mtu atakufa. JE NINI KITAENDELEA USIKOSE ......SURA YA ...22......

 INAPOENDELEA

Hali ile ilinifanya nikose amani, kwani wapangaji kama watano walihama kutokana na matatizo wanayokutana nayo,  kwa nyakati tofauti. Siku moja nilienda kanisani  kwenda kumueleza Mchungaji Mkombozi hali halisi ya mauzauza ya ile nyumba.Kutokana na matatizo yaliyokuwa  yanatokea, nilikuwa na wasiwasi huenda Mama Bilionea kuna vitu alivificha kule ndani hatukuviona. 

Nilipofika kwa Mchungaji nilimkuta akizungumza na kaka mmoja ambaye alionekana kuwa mgeni pale kanisani alinisalimia “Habari yako dada, mimi naitwa Charito sijui mwenzangu unaitwa nani,” Nilimtizama yule kaka alionekana mcheshi "Salama tu kaka mimi naitwa Kandida" Huku akitabasamu akanijibu "Nimefurahi sana kukufahamu Kandida" Hahahahahahah "Kilikuwa ni kicheko cha Mchungaji "Karibu Kandida, huyu kijana ni muumini mpya ambaye tutakuwa naye kanisani. Charito naona ulipomuona Kandida umeonyesha tabasamu pana sana" Alisema Mchungaji huku akimtizama Charito.

Nilisogea karibu na kuketi Charito alinyanyuka na kutoka nje na kutuacha mimi na mchungaji, nilimueleza kila kitu mchungaji akasema "Hapana, haiwezekani shetani kushindana na nguvu za Mungu, na hao wanaosema  bado kuna mambo ya kishirikina ni akina nani? Mimi namtumainia Mungu wangu pekee na naimani atapambana na nguvu yoyote ya giza" Aliongea mchungaji huku akiwa ananitizama. Tulianza kukemea palepale katika ofisi ya mchungaji na baadaye tukaenda pamoja katika nyumba ya Mama Bilionea safari hii tulikuwa pamoja na Charito. 

Sunday, June 16, 2013

DADA POA..DADA POA....DADA POA COMING SOON

Baada ya simulizi ya HAKUNA SIRI.... AMBAYO ITAISHA WIKI IJAYO......SIMULIZI YA DADA POA SI YA KUKOSA KUISIKILIZA HAPAHAPA KIJIWENI KWETU.

SIMULIZI ....KOSA LANGU NI NINI.....SURA YA ......7.......



 ILIPOISHIA
kesho ujiandae nitakupeleka Hospitali asubuhi kwenda kuitoa hiyo mimba" aliongea Maliki huku akiwa anaondoka na kumuacha Joyce akiwa analia pale sebuleni huku moyoni akiwaza "Kwanini mimi naishi maisha ya tabu hivi, nilijua Maliki ananipenda jamani nimemkosea nini Mungu laiti wazazi wangu wangekuwepo, sijui nitafanya nini na Maliki ndiyo anataka nitoe hii mimba si nitakufa mimi jamani" Alisema Joyce kwa uchungu. JE NINI KITAENDELEA... USIKOSE ...SURA YA ...7.....

INAPOENDELEA

Wakati huo ilikuwa mida ya saa nane za mchana. James mdogo wake na Joyce alikwa ametoka shule na kumkuta Joyce akiwa analia. James alishtuka kabla hata ya salamu alimuuliza "Dada unamatatizo gani? Mbona unalia kuna nini kimetokea" Dada yake alivuta kanga aliyokuwa ameivaa na kujifuta machozi huku akimwangalia mdogo wake kwa huzuni  "Hakuna kitu mdogo wangu nimewakumbuka sana wazazi wetu" Alisema Joyce ambaye siku zote alikuwa hapendi mdogo wake ajue kama anateseka.



  James alimshika mkono dada yake na kumwambia "Usilie dada hata mimi nawakumbuka sana lakini hatuna jinsi inabidi tumshukuru Mungu shemeji Maliki anatusaidia sana, bila yeye tungekuwa tunaishi mitaani."Akiwa anazungumza James alimkumbatia dada yake na baadaye aliingia chumbani kubadilisha nguo na kuendelea na mambo mengine.Siku hiyo ilikuwa ni siku mbaya sana kwa Joyce ambaye alikuwa hana amani muda wote alikuwa mwingi wa mawazo ilipofika usiku Maliki alirudi na kumkuta Joyce akiwa tayari amelala. Alimsogelea kwa umakini huku akiwa anamuangalia moyoni mwake aliwaza "Mmmmh leo nimegombana sana na huyu mtoto ngoja nimuamshe nimbembeleze".

 Alimsogelea tena kwa ukaribu zaidi na kumgusa paji la uso huku akimuamsha taratibu, Joyce aliamka na kumwangalia na macho yaliyokuwa yamelegea kutokana na usingizi. Maliki akamuambia embu amka tuzungumze kidogo, Joyce aliamka na kuketi kitandani.


LEO NI SIKU YA MTOTO WA AFRICA


WATOTO  KATIKA GARI WALILOTENGENEZA WENYEWE

WATOTO WAKIIMBA KWA FURAHA

WATOTO HAWA WANAHITAJI MSAADA ILI WAPATE HAKI YA MSINGI YA KUPATA ELIMU NA KUEPUKANA NA AJIRA ZA UTOTONI

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...