Sunday, May 20, 2012

SIMULIZI YA MAMA MDOGO SURA YA ...5.....


MTUNZI: ADELA DALLY KKAVISHE
KITABU  MALIPO NI HAPAHAPA KIPO MTAANI KWA SASA
EMAIL kavisheadela@yahoo.com
+2550652343430
ILIPOISHIA....“Usijali kuhusu hilo mpenzi, kwani mimi nilichoamua hakuna anayeweza kunipinga. Wewe ndiye utakuwa mama mwenye nyumba kuanzia sasa. Hapa ni kwako sawa mamaaa?” Alisema Mzee said kwa kujiamini huku akicheka.

INAPOENDELEA...Mzee Said aliamua kumtembeza Sophia pale nyumbani na kumwonyesha mazingira yote. Tangia siku ile Sophia aliishi na Mzee Said kama mke na mume na aliponogewa na mapenzi ya mke mpya aliamua kufunga ndoa harakaharaka bomani tena kisiri bila watu wengine kujua.

********
Siku moja Jamal aliomba ruhusa kwa mwalimu ili aende Hospitali kutokana na kusumbuliwa na homa.  Baada ya kuruhusiwa aliamua kwenda nyumbani ili akamtaarifu baba yake juu ya kuumwa kwake na kisha ampeleke hospitali. Ilikuwa ni siku ya Jumamosi, Jamal alijua lazima atamkuta baba yake nyumbani. Alipofika na kuingia getini, aliona gari la baba yake likiwa limepaki. Jamal alifurahi sana kwani alikuwa na uhakika kuwa baba yake yupo.
“Afadhali nimemkuta baba.” Aliwaza Jamal na kugonga mlango.

Baada ya kugonga mara kadhaa na kukosa majibu aliamua kuingia ndani na kuanza kuita.
“Baba! Baba!” Aliita Jamal lakini hakupata jibu.
Wakati huo baba yake alikuwa chumbani amepumzika na Sophia. Baadaye Mzee Said alisikia sauti ya Jamal ikiita kutoka sebuleni, alitoka haraka kuelekea sebuleni na kumkuta Jamal.

Tumia vipodozi asilia kutunza ngozi yako

ulaji wa chakula bora  ni miongoni mwa sababu kuu zinazochangia kuwa na ngozi yenye afya siku zote. Lakini ulaji huo, hufanya kazi vizuri zaidi kwa ndani, hivyo si vibaya na wewe ukafanya jitihada za makusudi katika kuhakikisha ngozi yako inakuwa na muonekano mzuri kwa nje.
Tango ,,Tunda hili linaweza  kupambana na kuchakaa na kuchoka kwa ngozi kunakosababishwa na tabia mbalimbali. Pia  lina uwezo mkubwa wa kusafisha ngozi hasa ya uso. Hiyo ni kazi moja kati ya nyingi zinazofanywa na tunda hili.
Unachotakiwa kufanya ni kusaga tango moja, kisha kuchuja juisi yake. Chukua pamba na chovya kwenye mchanganyiko wako kisha pakaa usoni. Kaa kwa muda wa dakika 20 hadi 30. Osha uso wako, kisha kausha kwa kitambaa safi na laini.Ikiwa juisi itakuwa nyingi, unaweza kuihifadhi kwenye jokofu kwa ajili ya matumizi ya siku za baadaye.


Pendelea kutumia vipodozi vya asili kuwa na ngozi ya asili isiyo na madhara

NAIPENDA NGOZI YANGU YA ASILI

Friday, May 18, 2012

SIMULIZI YA DADA YANGU SURA YA ....9,,,,,


KITABU  MALIPO NI HAPAHAPA 
MTUNZI  ADELA DALLY KAVISHE

LIPOISHIA,,,,,
“Lakini bora usilitumie kwani haya majina ya kurithi wakati mwingine sio mazuri unaweza ukampa mtoto jina la mtu mwenye mikosi na mtoto akajikuta anakuwa na mikosi katika maisha kwa sababu ya majina ya kurithi.” Alisema shangazi yake huku watu wote wakiangua vicheko.
 “Hakuna wifi hizo ni imani tu za watu.” Alijibu mama Upendo huku akiinuka kuelekea jikoni.
“Haya jamani huku jikoni vipi?” Aliuliza mama Upendo.
“Tayari mama hakuna tatizo.” Alijibu Upendo.

INAPOENDELEA,,,,,Waliendelea na mazungumzo pale sebuleni na baadaye baada ya kupata chakula cha usiku wote walikwenda kupumzika. Hatimaye siku ya sherehe ilifika, sherehe, iliandaliwa pale nyumbani kwa kina Upendo. Kulikuwa na uwanja mkubwa ambao ulipambwa vizuri sana. Ama kweli ilikuwa ni siku ya furaha kwa Upendo.

 Kwa upande wa mdogo wake Eliza mambo hayakuwa mazuri kwani muda wote alikuwa akiwaza sana kuhusu Juliasi kwa nini hapokei simu yake.
 “Eliza hii ni siku ya furaha ya maisha yangu naomba uwe na furaha mdogo wangu. Halafu leo pia ni siku mwafaka kwa wewe kumwona shemeji yako ambaye hujawahi kumwona, nadhani utampenda kwani nampenda sana.” Upendo alimfariji mdogo wake huku akimpigapiga mgongoni na kiganja cha mkono wake wa kulia.

Wednesday, May 16, 2012

JE SIMULIZI IPI UNAIPENDA ZAIDI je ni ya MAMA MDOGO, DADA YANGU AU KOSA LANGU,,,, IPI UNGEPENDA IENDELEE KWA HARAKA.

Asanteni sana kwa kuwa wadau wa simulizi zangu, ambazo naziweka kupitia hapa bloguni.Ningependa kufahamu kutoka kwako ipi unaipenda ambayo ungependa kufahamu muendelezo zaidi, pia unaweza kuweka mapendekezo nikuwekee muendelezo wa simulizi kila baada ya muda gani? tuko pamoja sana.

Katika hili unajikuta katika wakati mgumu sana

Picha hii nimeikuta Facebook ukweli mambo hayo yakikukuta inahitaji moyo hapo ndipo wengine wanakata tamaa ya maisha lakini ni vyema kupiga moyo konde na kufanya kazi kwa bidii

Ni muhimu kupata nafasi ya kupumzika baada ya kazi

Hilaly Sadalah wa PASSION FM RADIO akitafakari jambo

Kazi inaendelea "duuh leo nimechoka" sidhani kama kuna mtu anaweza kufanya kazi bila ya kupumzika ni vyema kutafuta muda wa kupumzisha akili ili kuboresha kazi yako wakati wote.

Pozi langu la leo

Ukijifinya mwenyewe hauwezi kusikia maumivu kama ukifinywa na mtu lol

Tuesday, May 15, 2012

WOMEN IN BALANCE KITCHEN PARTY GALA SEHEMU YA 3

INAKUJIA SOON SI YA KUKOSA

Mpenzi wangu anataka tendo la ndoa wakati nipo kwenye siku zangu

Mimi ni mwanamke ninampenda sana mume wangu tuna mwaka mmoja katika ndoa yetu hatujabahatika kupata mtoto nina tatizo ambalo ni kero ninazopata kutoka kwa mume wangu, tabia yake yakunitaka kimapenzi wakati nikiwa katika siku zangu naumia sana kwani nikimkatalia anasema simpendi wakati mwingine ananinunia mimi nampenda lakini tabia hii inanikera kiasi kwamba nakosa raha sijui nifanyeje naombeni ushauri

Thursday, May 10, 2012

Umuhimu wa kusherekea Sikukuu ya kina Mama (Mother's day)

Siku ya kina Mama Duniani huadhimishwa kila mwaka ifikapo tarehe 13 mwezi wa tano wewe kama Mama, mtoto,  na Baba unafikiri siku hii ina umuhimu gani kwako??,, mimi naamini Mama ni moja kati ya nguzo muhimu katika maisha yetu Siku hii ni muhimu kuwapongeza kina Mama wote duniani katika changamoto mbalimbali katika majukumu yake ya kila siku NANI KAMA MAMA.
Muandalie zawadi mama yako ama mama mlezi wako au Mama yeyote ambaye ungependa kumpa zawadi siku hii ni vyema kufanya hivyo MAMA NAKUPENDA,MAMA NI FURAHA NA UPENDO

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...