ILIPOISHIA
Upendo akiwa sambasamba na Eliza alielekea sehemu ile kwenye umati
wa watu ambako James alifichwa ili akamfichue. James akiwa katikati
ya
umati alimwona Upendo akiwa anatoka na pembeni akiwa na Esta
alishtuka sana kumwona Esta.
“Mungu wangu yule si Esta? Anafanya nini hapa na mbona yupo karibu
na Upendo? Kuna nini kinaendelea hapa?” James aliwaza na kujiuliza
maswali mengi yaliyokosa majibu.INAPOENDELEA
Kwa muda wa takribani dakika mbili hivi James alikuwa kama mtu
aliyechanganyikiwa. Watu waliendelea kushangilia huku James akiwa
hajui
nini cha kufanya baada ya kumwona Eliza ambaye ndio Esta akiwa
anatazama huku na kule kama vile mtu anayetafuta njia ya kutokea.
James akiwa anahangaika nini cha kufanya Upendo na Eliza waliendelea
kuangalia huku na kule wakimtafuta katika umati wa watu. Ghafla Eliza
akamwona Julias na kushtuka, lakini hakujua kama ndio mume mtarajiwa
wa dada yake.
“Haa! Hivi yule si Juliasi? Amefuata nini hapa? Au ni ndugu wa huyo
James? Mmh! Nina bahati kweli sikutarajia kumwona. Sasa hii ni nafasi
nzuri ya kuzungumza naye kuhusu hatima ya uhusiano wetu na hii mimba
yake.” Eliza alijiuliza maswali mengi huku akishangaa na kufurahi
kuonana
tena na Juliasi. Zoezi la kumfichua James halikufanikiwa kwani Upendo
alishindwa kabisa kumwona James alipokuwa. Hivyo waliamua kurudi na
kukaa katika sehemu maalumu iliyotayarishwa kwa ajili ya Upendo.









