Alipomaliza chuo tu Justa aliolewa na Mfaume kijana huyu alikuwa ni mfanyabiashara, ambaye alikuwa akimpenda sana Justa. Mfaume alikuwa akiishi na mdogo wake wa kike aliyekuwa anaitwa Leti kwa kipindi hicho Leti alikuwa bado anasoma chuo. Baada ya Justa kuolewa sasa alihamia na kuishi pamoja na mume na wifi yake, maisha yalikuwa mazuri kwani Mfaume alikuwa anampenda sana mke wake. Kwa kipindi hicho Justa alikuwa bado hajafanikiwa kupata kazi hivyo alikuwa ni Mama wa nyumbani huku akiwa anaendelea kutafuta kazi.
Siku zote Mfaume alikuwa akiacha pesa za matumizi pale nyumbani na alikuwa akimpa mdogo wake pesa hizo yaani hata pale mke wake alipokuwa na shida ilimbidi amweleze wifi yake kwani mume wake alikuwa akimpatia pesa zote za matumizi ya pale nyumbani mdogo wake.Hali ile ilikuwa inamuumza sana Justa na ndipo alipoamua kumwambia mume wake kuwa hapendezewi na tabia yake lakini mwanaume huyo hakutaka kumsikiliza. Siku zilivyozidi kwenda Justa alikuwa anakosa amani kabisa katika nyumba yake kwani alikuwa hana uhuru wowote kutokana na kila kitu alikuwa akipewa wifi yake.