Jumanne, Januari 24, 2012

Jamani wadau WOMEN IN BALANCE KITCHEN PARTY GALA mambo yameiva zimebaki siku chache kazi kwako hii siyo yakukosa wasichana na wanawake

Wasichana na wanawake wengi kwa sasa wanakabiliwa na changamoto nyingi sana ambazo zinapelekea kushindwa kusimama katika mahusiano yao.Teknolojia,mwamko wa elimu,wanawake kumiliki biashara binafsi,kazi,wazazi hawahusishwi ,kila mtu mjuaji ,kujisahau n.k
Matokeo yake talaka nyingi na mahusiano kuvunjika sasa tunataka kumkumbusha mwanamke wajibu wake na nafasi yake katika mahusiano.Ajitambue.
Msimu wa pili
Eneo hili limelenga kukuza ujuzi wa mwanamke  katika Nyanja za kijamii zaidi.Kupitia eneo  hili mwanamke atajifunza mambo mbalimbali kiasili na kisasa ambayo mwanamke anaengia au aliyeko  au anaetegemea kuingia katika mahusiano na ndoa.Mambo kama malezi  ya watoto ,nafasi yake katika jamii umuhimu kujiamini na mengineyo.
Wazo hili limekuja mara baada ya kuona kwamba ule muda wanawake wanaopata kuongea mambo haya kwenye kitchen party  ni mchache na hautoshi  kumfahamisha mwanamke mambo yote muhimu.Mambo  ambayo ni lazima ayajue au hata kama anayajua kutokana na pilika pilika za maisha anajisahau. 
Tukio hili kufanyika jumamosi hii ya tarehe 28 january 2012.Kuanzia saa nane mchana mpaka saa mbili usiku katika ukumbi wa Danken house uliopo mikocheni kwa warioba.
Watoa mada ni watu  wenye uwezo katika swala zima la uelimishaji 
Aunt sadaka;Ni mwana saikolojia aliyebobea katika maswala ya wanawake na watoto.Ana uwezo  katika Nyanja hii ambao umetokana kielimi na uzoefu wa kukutana na kesi mbalimbali amabazo zinazo mguza mwanamke hivyo kuweza kuwa funzo kwa wengine.
Bi Chau ni mwanamke ambae  mbali na kuwa katika fani ya sanaa kwa muda mrefu wamekua wakito amafunzokwa  wanawake tokea muda mrefu.Mafunzo ya mahusiano,ndoa na familia kwa ujumla.
Mama Victor;Ni mtumishi wa Mungu katika dini ya kikristo  ambae anaelimisha wanawake kwa mafunzo ya kidini.Anafundisha mwanamke  kujitambua vile mungu amempa uwezo wa kuitumikia jamii yake kama mlezi na kiongozi.
Kwa ufupi hawa ndio wakufunzi katika tukio letu hili la women in Balance jumamosi hii katika msimu wa pili.
Burudani itatolewa na Nyota Waziri.
Huu ni mkakati wa mwaka mzima huu 2012 na tutakutana kila mwezi mpaka mwezi march ambapo ratiba itabadilika na wanaume kuhusishwa.
WADHAMINI WETU WA SIKU HII NI
BAILEYS (kinywaji),MGen insuarance,cocacola,cooperate image na clouds fm.
IMETOLEWA NA MRATIBU WA WOMEN IN BALANCE
DINA MARIOS

Maoni 3 :

Bila jina alisema ...

hongera sana kw a waandaaji wamebuni kitu kizuri sana ningekuwa bongo ningefika huko

Bila jina alisema ...

yaani hii shughuli kuntu nimependa sana

Bila jina alisema ...

Dina, umependeza kwenye hizi picha, muno... mbona kwako hazipo tufaidi?

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

share bottom