Alhamisi, Machi 22, 2012

"Ni bora mwanamke kuwa mama wa nyumbani kuliko mwanamume kuwa Baba wa nyumbani na kusubiri kuletewa na mwanamke"

Anuary Sanga mtangazaji wa Radio Passion FM kipindi cha Drive Home Show amesema "yaani mimi naona ni bora mwanamke awe mama wa nyumbani kuliko mwanamume kwasababu mwanamume ni kichwa cha familia kwahiyo anatakiwa afanye juhudi ili kuitunza familia na tena ukiwa na mwanamke anafanya kazi halafu wewe umekaa nyumbani yaani hata kama anakupenda vipi ipo siku ataanza dharau, ujumbe wangu wanaume tuchangamke tufanye kazi kwa bidii kina Mama wako juu sana siku hizi.

Gosbert Njenga mtangazaji wa Passion FM kipindi cha Afro Passion yeye amesema "Mwanamume atabaki kuwa mwanamume hivyo ni vyema mwanamume afanye kazi na sio kujibweteka hata kama mke wako ana pesa kiasi gani na wewe jishughulishe ili kuweka heshima yako  mimi naamini mwanamke akiwa mama wa nyumbani ni kitu cha kawaida kwani analo jukumu la kulea watoto pamoja na mume wake na mwanamume kazi yake inakuwa ni kutafuta lakini itokee baba umekaa ndani halafu mwanamke ndiyo akatafute mimi kwangu sikubaliani kabisa, ijapokuwa inatokea hivyo labda mtu uwe ni mgonjwa  kiasi cha kushindwa kujishughulisha........haya jamani JE WEWE UNASEMAJE............

Maoni 1 :

lulu ibrahim alisema ...

dahhh sasa dada yangu kama ndio umeshapata mpenzi ambaye kazi hana mtaji hakuna na mwanamke mtaji pia wakumuweze hamna je itakuwaje utamuacha kisa yupo nyumbani na ukiangali kwa sasa asilimia kubwa ya wanaume waongo alafu unaona huyo ana nia kabisa na wewe je hapo inakuwaje dada adela

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

share bottom