Jumanne, Machi 27, 2012

Walimu wanaokiuka maadili ya kazi zao na kujiingiza kwenye mahusiano ya kimapenzi na wanafunzi, wanatakiwa kuwajibishwa.

Serikali imeshauriwa kuwawajibisha Walimu wanaokiuka maadili ya kazi zao na kujiingiza kwenye mahusiano ya kimapenzi na wanafunzi kutokana na kwamba hali hiyo inachangia kwa kiasi kikubwa kushuka kwa kiwango cha taaluma. Lakini pia kitendo hicho kinachochea kukosekana kwa maadili na hivyo kusababisha wanafunzi na walimu kutoheshimiana shuleni na kuchangia kiwango cha taaluma kuzidi kuporomoka. 

Ufike wakati sasa walimu wawajibishwe inapogundulika anajihusisha kimapenzi na mwanafunzi. Akizungumza na waandishi wa Habari Mwenyekiti wa wafanyabiashara wenye Viwanda na Kilimo mkoani Kilimanjaro  Bw Patrick Boisafi wakati akijibu maswali ya waandishi wa Habari waliotaka kujua nini kifanyike ili kukomesha tabia za walimu wenye mahusiano ya kimapenzi  na wanafunzi

Amesema baadhi ya walimu wamekuwa wakihamishwa vituo vya kzi pindi wanapobainika kufanya makosa hali ambayo hupelekea kosa hilo kuendelea hivyo ni vyema sheria ikachukua mkondo wake pindi mwalimu anapobainika kukiuka maadili na kuwa na mahusiano ya kimapenzi na mwanafunzi kwani tabia hii ipo kwa baadhi ya walimu ambapo ukikaa na kutafakari 

"Hivi kweli mwalimu akiwa na uhusiano wa kimapenzi na mwanafunzi anaweza kumuonya tena au kumuelekeza kitu akamuelewa ama kusikilizana au ndiyo kudharauliana. lakini pia wanafunzi wanatakiwa kusema kwa mzazi ama kumshataki mwalimu pale inapotokea anamtaka kimapenzi" JE WEWE UNASEMAJE......

Hakuna maoni:

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

share bottom