Jumatano, Machi 05, 2014

MADHUMUNI YA MAADHIMISHO YA SIKU YA WANAWAKE

Kila mwaka ifikapo tarehe nane mwezi wa tatu, Duniani kote wanadhimisha siku ya wanawake,  Mikoa yote nchini Tanzania imetakiwa kufanikisha siku ya wanawake. Madhumuni ya siku hiyo ni  ni kutoa fursa ya kupima utekelezaji wa maazimio, matamko na mikataba ya kimataifa, kikanda na kitaifa inayohusu masuala ya maendeleo ya wanawake na usawa wa kijinsia. Kwa mujibu Katibu Mkuu wa Wizara ya maendeleo ya Jamii, jinsia na Watoto, Anna Maembe  kauli mbiu ya maadhimisho  hayo ni "Chochea mabadiliko kuleta usawa wa kijinsia". Jamii itachochea mabadiliko ya kuachana na mila na desturi zenye madhara.

Hakuna maoni:

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

share bottom