Jumamosi, Machi 22, 2014

UJUMBE WA LEO NA RAIS WA TANZANIA JAKAYA MRISHO KIKWETE KWA WAJUMBE WA BUNGE LA KATIBA.

Akizindua rasmi Bunge maalaumu la Katiba jana mjini Dodoma aliwataadharisha wajumbe wa Bunge hilo kuwa makini kabla ya kuchukua uamuzi ambao unaweza kusababisha nchi kuingia kwenye hatari "Hii Serikali isiyo na uwezo, tegemezi ambayo haina dhamana, itakuwa inasimamiwa na wanajeshi ambao wakishindwa kulipwa mishahara baada ya miaka mitano wakavua magwanda na kupindua nchi" Alionya.

 Hata hivyo alisema "Watakachoamua Watanzania ni hichohicho wakiamua mbili tutakwenda huko huko, wakiamua tatu tukwenda lakini kweli serikali hii itasimama?.Alihoji na kuongeza "Suala la mfumo wa serikali tatu si jambo dogo ni lazima wawe makini kuamua.

Hakuna maoni:

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

share bottom