Jumatatu, Aprili 07, 2014

"Jay Z na Beyonce miaka sita ya ndoa na mapenzi motomoto"

Hivi karibuni Jayz na  Beyonce wamesherekea miaka 6 ya ndoa, kabla ya sherehe yao usiku, wawili hao walionekana wakitokea katika ofisi moja ya mjini New York huku Jay Z akiwa amembeba binti yao Blue Ivy.
Ndoa ya wasanii hao wawili wenye mafanikio makubwa kimuziki, imekuwa mfano kwa nyota , wengine ambao wamekuwa wakishindwa kudumu kwa japo miaka michache.Jay Z amekuwa akimsifia mke wake katika mambo mbalimbali ikiwa ni pamoja na kuendelea kuutunza uzuri wake ikiwemo  na umbo lake zuri la kuvutia.
Kila kitu kinawezekana, mnaweza kufurahia ndoa yenu hata miaka 50 na zadi cha muhumu ni uvumilivu, uaminifu, ubunifu na mapenzi ya dhati wakati wote katika shida na raha.

Hakuna maoni:

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

share bottom