Jumatano, Aprili 16, 2014

MANENO MAZURI KWA WAPENDANAO.....

"Usiwasikilize wale wasiopenda kuona wawili wakipendana, kumbuka tumependana wawili, unanifahamu vizuri zaidi yao, kama kuna jambo nimekukwaza usisite kuniambia mpenzi, nakupenda sana wewe ni ua la moyo wangu"
***********************************************************
"Ahadi yangu kwako ni kukupenda milele katika shida na raha, sintochoka kukupenda kwani ubunifu wako unanifanya nikuone mpya kila wakati najua unanipenda ndiyo maana upo tayari kwa lolote juu yangu na mimi nakupenda na nitakupenda milele"
***********************************************************
"Ninapoisikia sauti yako ya upole najisikia faraja moyoni mwangu, ukiwa mbali nami najihisi mpweke sana, ucheshi wako na tabasamu lako zuri lililojaa bashasha wakati wote linanikosha sana, natamani uwe karibu yangu wakati wote barafu wa moyo wangu."

Hakuna maoni:

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

share bottom