Ijumaa, Mei 16, 2014

MADHARA HAYA HUMKUTA MTOTO ANAYEANGALIA TV NA KOMPYUTA KWA MUDA MREFU.

Inaweza kuwa habari mbaya zaidi kwa watoto  lakini kitaalamu inaonyesha kuwa uangaliaji wa wa runinga kupita kiasi ni hatari kwa afya zao. Utafiti uliofanywa na chuo kikuu cha McGill cha Canada unaonyesha kuwa uangaliaji wa runinga na kompyuta kwa zaidi ya saa mbili unaweza kumsababishia mtoto kupata shinikizo la damu. Kwa mujibu wa wataalamu hali hiyo usababishwa na kukaa kwa muda mrefu  hivyo mwili kushindwa kufanya kazi yake ipasavyo ikiwemo mzunguko wa damu.
“Mtoto anapokaa muda mrefu kwenye luninga lazima atakuwa hapati muda wa kufanya mazoezi , kula vizuri na wakati mwingine kupata mapumziko ya kutosha , hivyo anakuwa kwenye hatari ya kupata shinikizo la damu, alisema mmoja wa washiriki wa utafiti huo,Dr. Ronald James . Utafiti huo ulikwenda mbali zaidi na kuonyesha mtoto mwenye shinikizo la damu yupo kwenye katika hatari zaidi ya kupatwa na maradhi ya moyo , maradhi ya figo na kupooza.

Maoni 1 :

emu-three alisema ...

Duuh, sasa itakuwaje maana huku kwetu sasa ni dampo la vilivyoshindikana, au uchafu wa kutupwa

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

share bottom