Ahadi ya kuwa pamoja maishani katika
 shida na raha,taabu na shida viapo hivi ama ahadi hizi zinaonekana 
kuchukuliwa kirahisi mno na wanandoa wapya, lakini kwa muujibu wa 
utafiti mpya uliotolewa hivi karibuni unathibitisha kuwa ni rahisi mno 
kutamka kuliko utekelezaji wa viapo vyenyewe .
Mtafiti uliofanywa 
kwa wanandoa wenye bahati 2,700 waliooana umegundua kwamba ,ikiwa 
mwanamke katika ndoa hiyo ataugua kwa muda mrefu asilimia sita hukaribia
 kupewa talaka kuliko wale ambao wana afya njema .
Ukilinganaisha 
na wanaume ambao huugua wakiwa kwenye ndoa,hatari ya kuvunjika kwa ndoa 
ni ndogo mno,hatahivyo upendo huendelea hadi hapo mmoja wao atakapo baki
 kuwa mgane ama mjane. Utafiti ulioongozwa na wanazuoni wa chuo 
kikuu nchini Marekani,kinapendekeza kwamba kwa asili, wanawake wao 
wameumbwa kutoa huduma katika familia zao nah ii inamaanisha kwamba 
wanaume wao huwa hawana uvumilivu wake zao pindi wanapokumbwa na maradhi
 ya muda mrefu ,ambayo pia yanweza kuwa hayatabiriki kuyakabili.
Walifanyiwa
 utafiti wanandoa nchini Marekani,ambao wote walikuwa na umri wa miaka 
50, mnamo mwaka 1990 ambao waliulizwa juu ya afya zao kuhusiana na 
maisha yao wakichnugza kwa miaka miwili,miwili ndani ya utafiti 
uliofanywa kwa miaka ishirini. Asilimia thelathini na mbili ya 
ndoa ziliishia kwa kuachana na asilimia ishirini na nnenzilivunjika 
kutokana na vifo vya mmoja wa wanandoa.
Kikosi cha utafiti 
kiliongozwa na Amelia Karraker, ambaye ni profesa msaidizi juu ya 
masuala ya maendeleo ya binaadamu na utafiti juu ya familia kutoka 
katika chuo cha Iowa State University,analinganisha matukio ya namna nne
 kansa,magonjwa ya moyo,kiharusi na magonjwa ya njia ya hewa kwa 
wanawake na wanaume na matokeo ya ndoa.
Utafiti huo 
umebainisha kwamba , kuna tofauti ya kujisikia mgonjwa sana na huwezi 
kupika chakula cha jioni, ama unahitaji mtu hasa wa kukulisha masuala 
haya yanaweza kubadili upepo ndani ya ndoa .
Katika hali 
hiyo,utafiti huo hauoneshi dhahiri kuwa mume ama mke anadai 
talaka,takwimu kamili zinaonesha kwamba wanawake ni wepesi zaidi kuomba 
talaka kuliko wenza wao.
Bi Karraker anasema amegundua kwamba 
kwamba inawezekana baadhi ya wanawake ambao huachwa kwasababu ya huduma 
zao ama kushindwa kuhudumia
Tafakari juu ya Uhai ama kifo 
husababisha watu wajitafiti wenyewe na kujiuliza maswali muhimu kuwa ni 
nini muhimu maishani mwao? Anaeleza mtafiti huyo.
Wanawake wakati 
mwingine huribuka kwa kusema kuwa waume zao hawawajali,na hawafurahishwi
 na suala hilo ama husema sikufurahishwa na mwanzo wa mahusiano yao, na 
wansema kwamba wako radhi kubaki peke yao kuliko kujitosa katika ndoa 
isiyofaa.
            

Hakuna maoni:
Chapisha Maoni