Jumatano, Januari 19, 2011

Baada ya mume wangu kugundua kuwa nina Virusi vya Ukimwi amenikimbia na kuniachia mtoto naishi katika mazingira magumu naombeni ushauri

Mimi ni msichana ambaye nilibahatika kuolewa nakupata mtoto wa kike mwaka jana mtoto akaanza kuugua mara kwa mara baada ya kupima akagundulika ana  virusi vya Ukimwi ,Baada ya mume wangu kufahamu mtoto ameathirika ametukimbia na mimi naishi katika mazingira magumu sana naombeni ushauri....

Nimepata ujumbe huo hakutaja jina lake ila amenipa namba yake ya simu kwa yule atakayehitaji kuwasiliana naye atawasiliana nami nitampatia.

Maoni 1 :

Bila jina alisema ...

POLE SANA NDUGU YANGU!
CHA MUHIMU KWANZA WEWE NI KUZITAFUTA ZILE CENTER AU ORGANIZATION ZA KUSAIDIA WATOTO WALIOATHIRIKA, ILI MTOTO APATE DAWA! NA WAO WATAKUELEKEZA SEHEMU YA WAKUBWA YA KUPATA DAWA ZA MISAADA, SABABU WEWE HAUJIWEZI! UNA HAKI YAKUSAIDIWA! MENGINE YOTE BAADAE!
FIGHT UPATE DAWA ZAKO NA ZA MTOTO NOW!

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

share bottom