Jumatatu, Januari 24, 2011

Wakati mwingine mtu anaweza kufanya mambo ya kukuumiza moyo na sio kwamba anafanya makusudi bali ni kujisahau kutokana na mapungufu yake ya kibinadamu

Unajua katika mapenzi unaweza ukaishi na mtu akakupa tabu sana,ila uvumilivu ni kitu cha busara,kwani inawezekana akakusumbua sana,akukera kutokana na mapungufu yake ya kibinadamu lakini bado unahitaji kuendelea kuwa naye maana licha ya kukukera ,ila anakupenda kwa dhati. kumbuka kuwa uvumilivu ni nguzo ya  pekee ili tuweze kufika mbali katika mahusiano ukizingatia kwamba hakuna marefu yasiyo na ncha.

Tusiachane jamani embu fikiria utaacha au kuachwa na wangapi kama ukiwa si mvumilivu,wakati mwingine mtu anaweza akakukera lakini hakukusudia bado anahitaji uwepo wako hivyo ni muhimu kumsaidia kutokana na matatizo aliyonayo huenda kuna siku ataelewa vipi aishi na mwenziye,ingawa inawezekana ikachukua muda mrefu hasa kama atakuwa hapendi kufanyia kazi ushauri wa mwenzake. UVUMILIVU NI WA MUHIMU KWANI VINGINEVYO HATUTAFIKA NA PIA NI MUHIMU KUYAGUNDUA MAPUNGUFU ULIYONAYO ILI UJIREKEBISHE.

Maoni 2 :

Simon Kitururu alisema ...

Tatizo watu wengi hawaongelei matatizo yao kitu kifanyacho kuwa bonge la kazi kustukia kiini cha mapungufu na kutibu hayo mapungufu!:-(

emu-three alisema ...

Hata gilasi kabatini hugongana sembuese sie wanadamu. Mnapokoseana ambizaneni na sameheaneni...!

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

share bottom