Jumanne, Juni 14, 2011

Maisha Mema Education & Training Centre wanakopesha waandishi wa vitabu

MaishaMema   Education & Training  Centre   ni  kituo  cha utoaji Elimu, Mafunzo, Utafiti  na  Ukuzaji Maarifa...Kituo  kinaratibu  mradi wa elimu  ya ujinsia  kwa  njia  ya  vitabu   kwa wanawake/wasichana  waliopo  mashuleni, vyuoni, magerezani  na  maofisini " SEXUALITY  EDUCATION & AWARENESS  PROJECT " mradi  ambao  umeanza  rasmi tarehe 1 JUNE 2011  kwa  kuwashirikisha  waandishi kumi na  tano ( 15 ) kutoka  katika  Chuo Kikuu cha Dar  es  salaam,  na  kwingineko.

Kituo   kinatoa  mkopo ( udhamini )    kwa  waandishi  wa  vitabu   wenye sifa  zifuatazo:
1.Jinsia  ya kike.
2.Umri  miaka  18  hadi  45.
3. Elimu  kidato  cha nne, sita  na  kuendelea.
4.Awe na  uwezo mkubwa  wa  kuandika  kitabu  ambacho kimefanyiwa  utafiti  wa kina juu  ya masuala  yanayo husiana  na ujinsia  miongoni  mwa  wanawake.( Kitabu chaweza  kuwa  cha  kiingereza  au  kiswahili ).....

Tutatoa  mkopo ( UDHAMINI )  juu  ya  gharama  za  uchapishaji  wa  kitabu  pia Tutakipeleka  kitabu  Sokoni..Baada  ya  kitabu  kuingia  sokoni, Tutarejesha  gharama   zetu za  mkopo pamoja  na  riba, kiasi   cha pesa  kitakacho baki  kitakuwa  ni mali ya mwandishi.

Fomu za  maombi  ya  mkopo  zinapatikana  katika ofisi  zetu  zilizopo  katika shule ya sekondari PERFECT VISION kwa  shilingi  Elfu Kumi  na Tano  Tu. ( Tshs.15,000/=).

Mwisho wa kutoa  fomu  za maombi  ya mkopo ni tarehe  17/06/2011.

KWA   MAELEZO  ZAIDI, WASILIANA  NASI  KWA SIMU  NAMBA: 0652458398  AU  0788363058

Au  tembelea  tovuti yetu : http://www.maishamematanzania.blogspot.com//

Hakuna maoni:

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

share bottom