Jumatano, Agosti 24, 2011

Ni muhimu kutunza siri za mapenzi kwa wapendanao.

Katika mahusiano ya kimapenzi ni lazima pawepo na siri baina ya wapendanao ili kuweza kulinda penzi lao lisipate hujuma kutoka nje, penzi ambalo halina siri yaani kila kinachofanyika ndani ya penzi lenu kinawekwa bayana kwa watu wengine basi hilo penzi haliwezi kudumu, kwani inakuwa rahisi mno watu kuwagombanisha, ogopa sana kuwa na mpenzi ambaye ni mpayukaji  kwani kila mtakalokuwa mnalifanya yeye atawaambia marafiki zake.

  katika kuwaambia marafiki wapo ambao watampa ushauri mzuri na wengine watampoteza kwa kumpa ushauri ambao hauna maana wala haujengi nakwahiyo utabomoa penzi lenu na kibaya zaidi kutoa siri za mapenzi ni kujiaibisha kwani mnawafanya watu wajue kila kitu kinachowahusu.NI VIZURI KUTUNZA SIRI KATIKA MAPENZI ILI KUWA NA UHUSIANO IMARA  VINGINEVYO UNAWEZA KUHATARISHA PENZI ULILONALO.

Maoni 1 :

emu-three alisema ...

Hilo nalo mpendwa, ...katika masharti ya ndoa hilo ni mojawapo, siri ya ndani ya ndoa kati ya wapendanao haisemwii nje...`ooh sijui hivi, kikashuka kikapanda..' unavunja miiko ya ndoa na `laana' itawaandama.
TUPO PAMOJA MPENDWA

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

share bottom