Alhamisi, Machi 01, 2012

"Nachukia tabia ya kaka yangu kunifuatilia na kugombana na marafiki zangu wa kiume"

Habari yako Adeladally mimi naitwa Salima ni mkazi wa Dar es salaam nipo kidato cha sita tatizo langu ni kuhusu kaka yangu ana tabia ya kumfuata kila mwanamume ninayeongozana naye na kumpa onyo asiwe karibu na mimi hiki kitu kinanikera sana kwani anasababisha mimi nakosa marafiki, nilishawahi kumuambia sipendi hiyo tabia akaniambia  atakuja kuwavunja miguu wanaume atakaowakuta karibu na mimi, ukweli ni kwamba huyo kaka yangu ndiye anayenilipia ada ya shule lakini sasa ananichunga hadi nakosa raha.

 nilikuwa na boyfriend wangu hivi majuzi alitukuta tumekaa tunazungumza alimshika yule boyfriend wangu na kumpiga sana na hadi hivi sasa yule boyfriend wangu hataki kuonana na mimi jamani sijui nimfanyeje huyu kaka yangu yaani hataki mimi kuwa na ukaribu na wanaume inaniboa sana.

Maoni 4 :

Bila jina alisema ...

At this age you think about boyfriends? shame upon U! Your bro is right coz is spending his masari to bring you up!Anyway le me ask what kind of relation do you 've with your Bf? Is it a passionate one? If it is in affirmative then your wrong! Your bro is grown up and knows the changing world but U dont know, so heed to your bro's concern! That is ALL!!! GOT IT?

Unknown alisema ...

salima ni kweli unayo yasema lakini kwa upande mwingine kaka yako yupo sahihi,kama atashindwa kukucotrol mapema hivyo mbeleni hutakuja kkushindikana be cool hayo mambo yapo utayakuta tu huwa hayaishi huba wewe piga kwanza book ctsa,just advers

Unknown alisema ...

Piga buku kwanza kama anavyotaka kaka yako, anakuandalia maisha yajayo tena anajisikia uchungu sana anapokuona unapotea wakati anajitahidi kukulipia ada kwa kile anachokipata, fuata taratibu zako mbona utazizoea tu!"Elimu kwanza dada, starehe baadae"

Bila jina alisema ...

Hata ningekuwa mimi ningefanya hivyo.Kaka yako anatumia pesa nyingi kukusomesha ili na wewe upate maisha mema baadaye.lakini wewe unakimbilia mambo ya kikubwa unataka kuharibu future yako na kupoteza pesa za kaka yako bure kwa kung'ang'ania mambo ya mapenzi?

Binti fumbuka, wanaume wapo utawakuta tu.Ukichanganya shule na mapenzi hutafika mbali.Ujue kuwa kaka yako anaona uchungu sana kukuona unataka kurubuniwa na wanaume wasiokuhusu hata kidogo.

Kama ni wema si wakulipie na ada ya shule ili kaka yako asitaabike bure.Waambie hao wanaume wakupe na pesa za ada na wewe uwape hayo mapenzi unayoyalilia.

Mtoto mdogo unadhiriki kusema kaka yako anakuboa wakati anapalilia maisha yako ya baadaye?Unadhani hao wanaume watakuoa au wanataka kula nyapu wakkuachie?Kwanza una bahati sana maana huyo kaka yako asingekuwa mwelewa kuwa wanaume wanadanganya mabinti na kuwaharibia maisha yao, angekushika wewe ndo ungepata hivyo vipigo badala ya hao wanaume.

Mpuuzi kabisa, eti mpenzi wangu amesema hatakuwa tena na mimi!! Una akili kweli?unaweza kutoheshimu kaka yako kisa mpenzi wako ndo awe wa maana na wakati kaka ndiye anakujengea future yako kwa kukuelimisha???Kaa chini na utulie bibie.Shule kwanza na mapenzi huko baadaye.

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

share bottom