Ijumaa, Julai 27, 2012

SIMULIZI YA MAMA MDOGO SURA YA 11....


KITABU MALIPO NI HAPA HAPA
MTUNZI ADELA DALLY KAVISHE

ILIPOISHIA ..... Jamal alilia sana, huku akimkumbuka marehemu mama yake. Hata hivyo aliamua kumwomba msamaha baba yake pamoja na mama yake mdogo, halafu akaelekea chumbani.
“Laiti mama angekuwepo haya yote yasingetokea, yaani baba ananipiga kwa sababu ya huyu mwanamke inaniuma sana.” Aliwaza Jamal na kuhuzunika sana.nini kinaendelea usikose sura ya 11.......

INAPOENDELEA...Kadiri siku zilivyozidi kwenda mama mdogo alizidisha visa na kuanza kumsingizia mambo ya uongo kwa baba yake. Kutokana na kusingiziwa na mama mdogo Jamal alikuwa akipigwa sana kila wakati hali iliyomkatisha tamaa Jamal. Jamal alitamani kutoroka lakini alivumilaia kwani alikumbuka
maneno ya mama yake mzazi alivyokuwa akimwambia kuwa zile mali ni zake pamoja na mdogo wake Aisha. Hivyo ilimbidi aendelee kuishi katika hali ya mateso.

Hatimaye matokeo ya Kidato cha Nne yalitoka na kwa bahati mbaya Jamal hakufaulu vizuri katika mitihani yake, kwani alipata daraja la tatu (division three). Hata hivyo kulikuwa na uwezekano wa kusoma shule binafsi. Kufuatia matokeo hayo Jamal alilia sana kwa uchungu kwani hata baba yake alimgombeza sana baada ya kuona kuwa amefeli ingawa mwanzoni aliahidi kumtafutia shule binafsi ili kuendelea na Kidato cha Tano.
Siku moja Jamal alikuwa amekaa chumbani kwake akijisomea kijitabu kimoja cha riwaya kiitwacho “Shija“. Ghafla aliingia mama yake mdogo na kuanza kumsemesha kama kawaida yake.


“Jamal mbona unanitesa hivi lakini? Ina maana hunielewi au hutaki kunielewa?” Aliuliza mama mdogo huku akikaa kwenye kitanda cha Jamal.
“Nilishakwambia siwezi kuwa na wewe. Kwanza najua wewe ndiye chanzo cha baba kunipiga bila sababu. Pili, kwa mila na desturi baba na mtoto wake hawawezi kuchangia mwanamke. Tatu sikupendi. Nne wewe ni Malaya. Tano unataka kuniharibia maisha yangu. Ila yote haya yataisha kwani karibia nakwenda zangu shule.” Aliongea Jamal kwa mama yake
mdogo huku akirusha mikono kama anasoma ngonjera.

“Unajiona mjanja, baba yako atakupeleka shule nikiamua hata hiyo shule huendi.” Alijibu mama mdogo huku akicheka kwa dharau. “Inamaana mama mdogo yote unayonifanyia unaona haitoshi na sasa unataka hata kunizuia nisiende shuleni? Nakwambia shuleni nitakwenda na huwezi kupinga hata kidogo.” Aliongea Jamal kwa kujiamini. “Tutaona nani mjanja.”Alisema mama yake mdogo na kubamiza mlango
na kuondoka.

Baada ya siku tano kupita tangia mama mdogo na Jamal wajibizane maneno ya kukashifiana, mama mdogo alifikiria na kubuni njia nyingine ya kumfanyia visa Jamal.
“Sasa hebu nibuni kisa ambacho baba yake akisikia tu hata nia ya kumpeleka shule Jamal itakufa. Mwanamke siku zote ni mjanja kupita mwanamume. Na mbinu hii ni komesha.” Aliwaza mama mdogo.
“Nitamtafuta mwanamke na kumweleza yote kuhusu ninavyompenda Jamal, na jinsi kijana huyu anavyonisumbua. Kisha nitamwomba aniandikie ujumbe wa uongo utakaoonyesha Jamal ameandikiwa na mwanamke, halafu nitampa baba yake ili akiusoma asimpeleke shule. Nafikiri hapo nitakuwa nimempata.” Aliwaza mama mdogo.
Baada ya kupata hilo wazo mama mdogo alifanya hivyo na kisha kumpelekea ile barua baba yake na Jamal. Siku hiyo baba Jamal aliwahi kurudi nyumbani na kumkuta mke wake amekaa sebuleni akimsubiri. Jamal yeye alikuwa amekaa chumbani kwake.

“Mume wangu hii bahasha ndani ina ujumbe kuna msichana ameiletanimpe Jamal nimefungua nikasoma niliyokutana nayo nimeshindwa kuamini macho na akili yangu nimeona nikupe kwanza uisome uone mambo anayofanya mtoto wako.” JE NINI KITAENDELEA USIKOSE SURA YA 12


Maoni 3 :

Bila jina alisema ...

mhhhhhhhh htr ila unatutendaje sasa?mna kila ck tunafungua hkn kitu.

Bila jina alisema ...

we ma mdogo una tabia mbaya sikupndiiii

Bila jina alisema ...

Habari Debby, naifurahia kazi zako big up kweli wanawake tunaweza without kuwezeshwa, sina comment kuhusu kinachoendelea hapo juu ila nia yangu ni kujua kabila ambalo mwanamke anatakiwa kutembea na shemeji zake zote according to your program uliyoirusha passion radio pliiiiiiz naomba uniambie.

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

share bottom