Jumanne, Desemba 11, 2012

SIMULIZI YA MAMA MDOGO SURA YA .....18.......





ILIPOISHIA
Akasogea karibu na baba yake akapiga magoti mbele yake huku machozi yakimtoka. “Baba nimekukosea sana! Nimetenda dhambi kubwa mbele za Mungu pia. Nisipotubu dhambi hii sitapona nitateseka maisha yangu yote…”
Jamal aliongea kwa huruma na huzuni kubwa. Baba yake alimsikiliza Jamal kwa makini na huku mama yake mdogo akimwangalia na kuwaza moyoni mwake ni nini anataka kusema Jamal. Aliingiwa na hofu kubwa sana. JE NINI KINAENDELEA USIKOSE SURA YA .......18..........

INAPOENDELEA:
“Baba unakumbuka wakati ule mama mdogo alipokupa ule ujumbe ambao ulionyesha kuwa nimeandikiwa na msichana anaitwa Mary na ukanichukia sana hadi ukakataa kunipeleka shule.” Alieleza Jamal. “Ndio nakumbuka Jamal lakini nilishakusamehe mwanangu.” Alijibu baba Jamal. “Baba haikuwa kweli zilikuwa ni njama za mama mdogo kwani alikuwa akinitaka kimapenzi nilipokataa ndipo akanitafutia sababu nyingi ili unichukie.” Aliongea Jamal huku akimwangali mama yake mdogo.

“Hivi wewe Jamal una kichaa au! Unasema nini?” Alihamaki na kufoka mama mdogo huku akisimama kumfuata Jamal kwa hasira. Baba Jamal alimtaka anyamaze ili Jamal aendelee kuzungumza. Jamal alisimulia matukio yote yaliyotokea kuanzia mwanzo hadi mwisho. “Naomba unisamehe baba haikuwa kusudio langu. Kibaya zaidi baba…” Jamal alishindwa kuendelea baada ya mama yake mdogo kumkonyezakuashiria asiseme.
“Eleza yote mwanangu. Eh! Kibaya zaidi nini?” Aliuliza baba yake. “Kibaya zaidi hata huyu mtoto Rama si…” Mama mdogo alimziba mdomo Jamal.


Baba Jamal alisimama na kumpiga kibao mama mdogo hadi akaanguka chini. “Mwache aseme yote, kama siyo kweli kwanini unamzuia asiseme?” Alifoka baba Jamal huku amemkanyaga mama mdogo. Aisha alimkimbilia Rama na kumchukua na kwenda naye nje. “Baba hata huyu mtoto si wako nilimpa mimba mama mdogo kipindi kile uliposafiri miezi miwili. Nakuomba unisamehe sana baba.” Aliongea Jamal huku ameshika miguu ya baba yake na kulia kwa uchungu.

“Hivi wewe Jamal umepona kweli au bado unaumwa? Ni mambo gani haya unayoyasema? Siamini! Utakuwa haujapona vizuri Jamal, mambo haya ni mazito sana, mwanangu.” Aliongea baba Jamal huku akimwangalia Jamal na kisha mama mdogo. “Naongea kweli kutoka moyoni,, baba naomba unisamehe. Nakuomba umuulize mama mdogo aseme ukweli ulivyokuwa.” Alimaliza kuongea Jamal. Baba Jamal alimgeukia Jamal na kumpiga kibao ambacho kilimfanya ahisi kizunguzungu na kuanguka chini huku anapiga kelele.“Ananiua! Ananiua!.” Jamal alilalamika.

“Nyamaza mpumbavu mkubwa wewe!” Alifoka baba Jamal. Kisha alimshika mkono mama mdogo na kumuuliza yote aliyosema Jamal kama ni ya kweli. “Nakuuliza wewe kinyago anayosema Jamal ni ya kweli?” Alifoka baba Jamal huku midogo ikimchezacheza kwa hasira. “Ni kweli! Naomba unisamehe.” Alijibu mama mdogo huku akitetemeka mwili mzima. Baba Jamal alimpiga mama mdogo vibao visivyo na idadi kimyakimya bila kusema neno lolote. Wakati mama mdogo akiendelea kupokea kipigo, Jamal alinyanyuka kisirisiri na kukimbilia nje. 

Baada ya baba Jamal kumpiga sana mama mdogo aliingia chumbani na kufunga mlango kwa ndani. Akiwa ndani alichukua karatasi mbili moja aliandika ujumbe ufuatao na kuweka juu ya meza: “Mungu nisamehe Siwezi kuvumilia hii aibu Naomba uipokee roho yangu.” Karatasi ya pili akaandika ujumbe mwingine na kuiweka katika moja ya suruali zake na kutupa chini ya uvungu wa kitanda. Alipomaliza kuandika ujumbe alielekea katika kabati lake na kuchukua bastola yake kisha kuielekeza kifuani na kuifyatua.

Mama mdogo aliposikia mlio wa bastola aliinuka na kuelekea chumbani na kukuta mlango umefungwa. Mama mdogo alimwita Jamal na Aisha haraka ambao walikuwa nje wakiendelea kulia. Jamal na Aisha waliingia na kukuta mama yao mdogo akihangaika kumwomba baba yao afungue mlango. “Baba fungua! Baba fungua mlango!” Aliita Jamal. Wakati Jamal anaendelea kumwomba baba yake afungue mlango, Aisha aliendelea kumbembeleza Rama ambaye muda wote alikuwa akilia. Mama mdogo aliamua kukimbia na kutokomea kusikojulikana.

Jamal aliamua kupiga simu polisi ambao walifika haraka na kuvunja ule mlango na kumkuta baba Jamal akiwa amelala pale chini tayari alikuwa amekufa. Jamal na Aisha walilia sana huku wakimkumbatia baba yao kwa uchungu. Polisi walianza kuhoji chanzo cha tafrani ile, Jamal alipoanza kueleza ndipo alipogundua kuwa mama mdogo hakuwepo. Wote walianza kumtafuta mama mdogo katika vyumba vyote lakini hakuonekana. Walikwenda nyumba za jirani hakuwepo. Ikawa ni tafrani mpya ya kumtafuta mama mdogo hadi apatikane.

 Umati wa majirani na watu kutoka mitaa mbalimbali ulizingira nyumba ya akina Jamal ili kujua kulikoni. Pamoja na umati mkubwa wa watu kusaidia kumtafuta mama mdogo hakuweza hakupatikana. Polisi waliamua kuuchukua mwili wa baba Jamal wakati uchunguzi wa chanzo cha tukio ukiendelea. USIKOSE SURA YA 19.........






Maoni 3 :

Thiet ke logo alisema ...

This is very useful for me.Can you share with us something more like this. Thanks.

Unknown alisema ...

This is very useful for me.Can you share with us something more like this. Thanks.

Unknown alisema ...

Natafuta 19 na 20 mbona sioni ?

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

share bottom