Alhamisi, Mei 22, 2014

MANENO MAZURI KWA WAPENDANAO

"Mapenzi yako ni kila kitu katika maisha yangu, napenda unavyonijali na kuniheshimu, siku zote umekuwa ukiniongoza na kunipa mawazo mazuri katika changamoto za maisha, nakupenda sana mpenzi wangu tupendane milele"
***********************************************************************
"Nahisi baridi na homa kali unapokuwa mbali yangu, natamani nikuone au nisikie sauti yako wakati wote, wewe ni furaha ya maisha yangu nakupenda sana, nafurahi zaidi kupendwa na wewe chaguo la maisha yangu"
************************************************************************
"Nasikiliza moyo wangu naamini unanieleza ukweli kuwa wewe ni wa kwangu peke yangu, siwezi kusikiliza maneno ya watu nakupenda nakuamini, Mungu atujalie tupendane milele"

Hakuna maoni:

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

share bottom