Jumatatu, Oktoba 20, 2014

UJUMBE WA LEO "TABASAMU WAKATI WOTE HATA KAMA MOYO WAKO UNAVUJA DAMU ILI UISHI NA KILA MTU VIZURI"


Binadamu wakikukwepa usijali, ipo siku watakutafuta, wakikusengenya nyamaza huenda watajifunza wakikununia omba Mungu ipo siku watakuchekea, wakikupongeza usiwaamini labda wanakudhihaki, wakikutenga achana nao, wao sio kila kitu, wakikudhulumu shukuru Mungu atakulipa, na wakikualika kuwa makini isije ikawa wanataka kukutega , uwe muangalifu kwa kila jambo halafu onyesha tabasamu hata kama moyo unavuja damu, ili uishi na kila mtu vizuri.

Maoni 2 :

emu-three alisema ...

Kweli ujumbe murua chukulia kama kila mtu angalifanya hivyo, dunia ingelikuwaje, ni raha, tabasamu upendo na amani kwa saana, ubarikiwe mpendwa kwa ujumbe huu. Tupo pamoja

Amor alisema ...

Safi sana. Huu ujumbe imetulia sana.

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

share bottom