Jumamosi, Januari 03, 2015

PENDELEA KULA BAMIA KUJENGA AFYA YA NGOZI

Bamia ina majina lukuki, wengine huiita okra, kwa jina lisilo rasmi la Kiingereza huitwa, ‘lady finger’ au gumbo. Bamia ni miongoni mwa mboga za majani ambazo kwa kisayansi huitwa, ‘Abelmoschus Esculentus’

Vitamini A itokanayo na bamia husaidia kuupa mwili wako kinga ya kupigana na maradhi.  Kwa wenye matatizo ya kuona, kula bamia mara kwa mara kutaimairisha mwanga katika macho yako.
Wingi wa vitamini A huzuia maradhi  yatokanayo na virusi kama mafua.

Uteute uliomo katika bamia husaidia kuunda tishu za mwili na ngozi. Watu wenye ngozi laini na zinazoteleza wana kiwango kikubwa cha ute ambacho husaidia kujenga ngozi.

Ulaji wa mboga za majani kama bamia, husaidia katika kulinda mapafu na saratani za mdomo.  Bamia zina wingi wa vitamini K ambayo husaidia kuimarisha mifupa na kuganda kwa damu.

Maoni 1 :

Unknown alisema ...

Ahsante,lakin naomba kujua jinsi ya kutayarisha hzo bamia??

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

share bottom