Jumatatu, Oktoba 14, 2013

SIMULIZI YA KOSA LANGU NI LIPI SEHEMU YA ...........20...........


ILIPOISHIA 
Joyce aliinama chini kwa aibu "Mama naomba unisamehe sikukusudia kutenda yote haya ni shetani tu alinipitia nisaidie mama ni wewe pekee unaweza kuwa karibu na mimi" waliendelea kuzungumza baadaye mama Robert alinyanyuka na kuelekea chumbani huku akimtaka Joyce aende chumbani kwake akapumzike. ITAENDELEA 

INAPOENDELEA
Huko chumbani Joyce alikuwa akiwaza "Eeee Mungu naomba unisaidie sijui Baba mkubwa akija atanifanya kitu gani, si anaweza kunifukuza hapa nyumbani,  sijui nitaenda wapi mimi".

Nyumbani kwa  Sukari alikuwa akiishi na dada zake ambao ndiyo walikuwa wakimuangalia mtoto wa Joyce mmoja alikuwa akiitwa Samanda na mwingine aliitwa Sungi siku hiyo walikuwa wamekaa pamoja kibarazani wakiteta "Ndugu yangu Samanda hivi ukimuangalia huyu mtoto wa kaka unamuonaje?" Aliuliza Sungi "Mmmh na wewe kwani amefanyaje mi naona ni mtoto mpole hana matatizo kwani wewe unamuonaje".

 Alijibu na kuuliza Samanda huku akiguna kidogo, Sungi akaendelea kusema "Yaani mimi huyu mtoto nikimuangalia tu naona kama si wa kaka yetu kabisa mbona hata hafanani naye. "Huo sasa ni umbea ndugu yangu mimi naona kawaida tu acha mambo ya kizamani kwahiyo asipofanana naye ndiyo unamaanisha kuwa yawezekana kuwa huyu siyo mtoto wake" Alihoji Samanda "Ndiyo, huyu mtoto siwakwake kaka amekurupuka tu" Sungi aliongea huku akijiamini. "Hee! Wewe Sungi umechanganyikiwa,  tena nyamaza kaka asije kukusikia kwasababu anaweza hata akakufukuza hapa nyumbani".


 Wakiwa wanaendelea na mazungumzo Sukari alifika na kuwakuta lakini hakuwasikia walichokuwa wanazungumza "Habari za kushinda" "Salama tu kaka pole na kazi" Huku Sungi  akinyanyuka na kumpokea mfuko aliokuwa ameweka zawadi za mtoto James. Maisha yaliendelea huku Joyce akiwa hajui nini muskabali wa maisha yake na alimfikiria pia Baba yake mkubwa akigundua itakuwaje."Yaani najuta sana, kutenda kosa hili, Baba mkubwa akijua nahisi atanifukuza nyumbani kwake eeh Mungu nisaidie".

 Ikiwa takribani kama wiki mbili tokea mtafaruku wote huo utokee Joyce akiwa anaendelea kuishi nyumbani kwa Baba yake mkubwa bila amani kutokana na kuwa na mawazo sana alimkumbuka mtoto wake.Wakati wote huo Baba Robert alikuwa hayupo.

Siku moja Mama Robert akiwa  ameketi Sebuleni akitizama tamthilia  huku akiwa hana hili wala lile, mara ghafla Robert aliingia "Mama Mama eeh  Mungu wangu" Aliongea Robert kama amechanganyikiwa Mama  yake alimshangaa kumuona katika hali ile,  na kumuuliza "Wewe unawazimu? ni kitu gani, embu tulia kuna nini? "Baba amefariki Mama Baba amegongwa na gari Mama"Robert alionekana kutetemeka huku kijasho chembamba kikimtoka katika paji la uso wake aliongea moja kwa moja huku  Mama yake aliyekuwa ameketi alinyanyuka kwa mshtuko "Eti unasema nini wewe? eeeh ni nini, ajali nani eeh Mungu wangu".

 Ghafla Mama Robert aliishiwa nguvu akaanguka  chini na kupoteza fahamu. Joyce alikuwa kama amepigwa butwaa asijue nini cha kufanya huku akimtizama Robert "Wewe Robert umefanya nini jamani, angalia sasa Mama ameanguka, Mama, Mama, amkaMama" aliongea kwa sauti iliyojaa wasiwasi mwingi. Lakini Mama Robert alikuwa amezimia kwa mshtuko alioupata. Robert na Joyce  walikimbia kwa majirani kuomba msaada. Walikuja na haraka walimbeba Mama Robert kisha kumpeleka Hospitalini. 

Baba robert alikuwa amepata ajali mbaya iliyosababisha kifo chake palepale wakati akiwa anatokea safarini kurudi nyumbani. Vilio na majonzi vilitawala katika familia ya kina Joyce taratibu za mazishi zilianza huku Fredy akimsaidia Joyce na kusahau tofauti zilizopo baina yao kwani kwa wakati huo Joyce alikuwa katika wakati Mgumu na hata kwa upande wa Fredy Baba Robert alikuwa ni kama Baba yake mzazi.

 Joyce alikuwa analia kwa uchungu huku moyoni akiwaza "Eeh Mungu nakuomba umsaidie Mama arudi katika hali yake ya kawaida. Ni balaa gani hili jamani Baba mkubwa ndiyo ametutoka, Mama naye hali yake siyo nzuri. Matatizo yamekuwa mengi "Akiwa anaendelea kuwaza Fredy aliyekuwa anatembea huku na kule kutoa pole kwa ndugu jamaa na marafiki alimuona na kusogea karibu.

 "Pole Joyce kwa matatizo ni mapenzi ya Mungu.Sisi tulimpenda lakini Mungu kampenda zaidi" Fredy alikuwa akimfariji, Joyce alikuwa akibubujikwa na machozi "Inaniuma sana Fredy siamini kama Baba mkubwa amefariki na hali ya mama hospitalini bado si nzuri” Aliongea kwa uchungu huku akimtazama Fredy aliyekuwa akimfariji, Huko Hospitalini   hali yaMama Robert iliendelea kuwa mbaya kwani kipindi chote hicho alikuwa hajitambui.Kutokana na presha kuwa katika hali mbaya sana  iliwabidi waendelee na taratibu za mazishi hivyo Baba Robert alizikwa bila hata ya mke wake kuhudhuria.


Baada ya wiki moja tokea Baba Robert apumzike kwenye makazi yake ya milele, Joyce pamoja na Robert waliendelea kwenda Hospitalini ili kumjulia Mama hali “Mgonjwa anaendeleaje Daktari” Joyce alimuhoji Daktari aliyekuwa akimuhudumia Mama Robert , “Karibuni ofisini mgonjwa amepumzika mnaweza kuzungumza naye hapo baadaye.  ITAENDELEA 

Maoni 2 :

Bila jina alisema ...

joyce mwaya pole.

Bila jina alisema ...

dada adela samahani ujue namesoma hii story lkn nimetatufa part 1 na nyinginezo napata nusunusu hebu nambie nifanyeje nianze mwanzo wa story hiii mpaka mwisho?

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...

share bottom