ILIPOISHIA
Joyce aliinama chini kwa aibu "Mama naomba unisamehe sikukusudia kutenda yote haya ni shetani tu alinipitia nisaidie mama ni wewe pekee unaweza kuwa karibu na mimi" waliendelea kuzungumza baadaye mama Robert alinyanyuka na kuelekea chumbani huku akimtaka Joyce aende chumbani kwake akapumzike. ITAENDELEA INAPOENDELEA
Huko chumbani Joyce alikuwa akiwaza
"Eeee Mungu naomba unisaidie sijui Baba mkubwa akija atanifanya kitu gani, si anaweza kunifukuza hapa nyumbani, sijui nitaenda wapi mimi".
Nyumbani kwa Sukari alikuwa akiishi na dada zake
ambao ndiyo walikuwa wakimuangalia mtoto wa Joyce mmoja alikuwa akiitwa Samanda
na mwingine aliitwa Sungi siku hiyo walikuwa wamekaa pamoja kibarazani wakiteta
"Ndugu yangu Samanda hivi ukimuangalia huyu mtoto wa kaka unamuonaje?" Aliuliza Sungi "Mmmh na wewe kwani amefanyaje mi naona ni mtoto mpole hana
matatizo kwani wewe unamuonaje".
Alijibu na kuuliza Samanda huku akiguna kidogo, Sungi
akaendelea kusema "Yaani mimi huyu mtoto nikimuangalia tu naona kama si wa
kaka yetu kabisa mbona hata hafanani naye. "Huo sasa ni umbea ndugu yangu
mimi naona kawaida tu acha mambo ya kizamani kwahiyo asipofanana naye ndiyo
unamaanisha kuwa yawezekana kuwa huyu siyo mtoto wake" Alihoji Samanda
"Ndiyo, huyu mtoto siwakwake kaka amekurupuka tu" Sungi aliongea huku akijiamini. "Hee! Wewe
Sungi umechanganyikiwa, tena nyamaza kaka
asije kukusikia kwasababu anaweza hata akakufukuza hapa nyumbani".












