ILIPOISHIA
Nilikuwa nawaza huku Renata
akinitikisa mkono kwa nguvu na kunivuta “Dada twende tukamtafute Tumaini,
twende dada” Wakati huo Charito alikuwa amesimama pembeni na kusema
“Inawezekanaje mlinzi alikuwepo hapa getini halafu mtoto anakimbia anashindwa
kumrudisha, sasa atakuwa amekimbilia wapi, si unajua Dar es salaam ni kubwa”
Alisema Charito huku akiwa anaelekea kumtafuta mlinzi na mimi nikawaza kuwa
hawezekani Tumaini akawa ameenda sehemu
ya mbali labda atakuwa maeneo ya karibu, haraka nilitoka nje na kuanza
kuwauliza majirani JE NINI KITAENDELEA USIKOSE...... SEHEMU YA........28.........
INAPOENDELEA
Nilizunguka
huku na kule kumtafuta Tumaini bila ya mafanikio. kwani kila jirani nileyekuwa
nikimuulizaa alisema hakumuona Tumaini.Nilikuwa na mawazo sana huku nikiwa na
hisia labda Tumaini anaweza kupotea kabisa au hata kugongwa na gari.Wazo la
kwenda kuripoti kituo cha polisi sikuwa nalo kabisa kichwani niliendelea
kuzunguka huku na kule na machozi yalikuwa yakinilengalenga kutokana na hofu ya
kuwa naweza nisimpate mdogo wangu.
Kwa wakati
huo mume wangu naye alikuwa akizunguka kumtafuta Tumaini.Yalipita masaa kama
matatu huku tukimtafuta Tumaini bila ya mafanikio ilinibidi nirudi nyumbani
huku mawazo yangu yakinipelekea kuwa yawezekana Tumaini akarudi mwenyewe.
Nilipofika nyumbani nilimkuta mume wangu akiwa ameketi sebuleni pamoja na Renata "Vipi jamani, inamaana Tumaini hajarudi nyumbani" Charito alinitizama na kusema "Nimehangaika sana kumtafuta huku na kule bila ya mafanikio nilifikiri labda wewe utakuwa umempata, sasa sijui atakuwa ameelekea wapi" Wakati Charito akiwa anazungumza Renata alimtizama Charito na kusema kwa sauti iliyojaa hasira kali "Wewe shemeji unajua wapi ameenda Tumaini, sema yuko wapi mdogo wangu?".